2015-01-03

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

Sekretariati ya Ajira katika Utumishi wa Umma ni chombo ambacho kimeundwa kwa mujibu wa Sheria ya Utumishi wa Umma Na. 8 ya mwaka 2002 kama ilivyorekebishwa na Sheria Na. 18 ya mwaka 2007 kifungu 29(1). Kwa mujibu wa Sheria hiyo, chombo hiki, pamoja na kazi zingine kimepewa jukumu la kutangaza nafasi wazi za kazi zinazotokea katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Waajiri (Taasisi za Umma).
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma anakaribisha maombi kwa Watanzania wenye sifa na uwezo wa kujaza nafasi 593 za kazi kwa ajili ya wakala wa vipimo kama zilivyorodheshwa katika tangazo hili.
NB: MASHARITI YA JUMLA KWA KAZI ZOTE.
i. Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania na wenye umri usiozidi miaka 45
ii. Waombaji wote waambatishe cheti cha kuzaliwa.
iii. Waombaji ambao tayari ni watumishi wa Umma na wamejipatia sifa za kuingilia katika kada tofauti na walizonazo, wapitishe barua zao za maombi ya nafasi za kazi kwa waajiri wao na Waajiri wajiridhishe ipasavyo.
iv. Nafasi ya kazi inayoombwa iandikwe juu ya bahasha, kutozingatiwa hili kutasababisha maombi ya kazi kuwa batili.
v. Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye anwani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini (referees) watatu wa kuaminika.
vi. Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma, maelezo, nakala za vyeti vya kidato cha nne na kidato cha sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu
mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika. Viambatanisho hivyo vibanwe sawa sawa kuondoa uwezekano wa kudondoka au kupotea.
- Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Diploma/Certificates.
- Cheti cha mtihani wa kidato cha IV na VI
- Computer Certificate
- Vyeti vya kitaaluma (Professional certificates from respective boards)
- Picha moja “Passport size” ya hivi karibuni iandikwe jina kwa nyuma.
vii. Testmonials”, “Provisional Results”, “Statement of results”, hati matokeo za kidato cha nne na sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS) HAVITAKUBALIWA.
viii. Waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na Mamlaka husika (TCU na NECTA).
ix. Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wanakibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.
x. Waombaji kazi ambao tayari ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko katika Utumishi wa umma wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika Waraka Na CAC. 45/257/01/D/140 wa tarehe 30 Novemba 2010.
xi. Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kugushi wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.
xii. Mwisho wa kupokea barua za maombi ni tarehe 18 Januari, 2015
xiii. Aidha, uwasilishaji wa barua kwa mkono katika ofisi za Sekretarieti ya ajira HAURUHUSIWI.
xiv. Maombi yanaweza kuandikwa kwa Lugha ya Kiswahili au Kiingereza na yatumwe kupitia posta kwa anuani ifuatayo.
Katibu, AU Secretary,
Sekretariati ya Ajira katika Public Service Recruitment
Utumishi wa Umma, Secretariat,
SLP.63100, P.O.Box 63100
Dar es Salaam. Dar es Salaam.
1.0 WAKALA WA VIPIMO
Wakala wa Vipimo ni Taasisi (Wakala) ya Serikali iliyochini ya Wizara ya Viwanda na Biashara. Taasisi hii iliundwa kwa mujibu wa Sheria ya Wakala za Serikali Sura Na. 245, mapitio ya mwaka 2002. Wakala wa Vipimo ilianzishwa rasmi tarehe 13 Mei, 2002 kwa amri ya Serikali Na. 194 (Government Order No. 194) na kutangazwa tarehe 17 Mei, 2002. Wakala wa Vipimo ina jukumu la kumlinda mlaji kwa kuhakiki vipimo vyote vinavyotumika katika sekta za Biashara, Afya, Usalama na Mazingira.
Nafasi hizi zitajazwa katika ofisi za Wakala wa Vipimo zilizoko Makao Makuu na katika Mikoa yote Tanzania Bara.
1.1 AFISA UGAVI MKUU DARAJA LA I - NAFASI 1 (INARUDIWA)
1.1.2 MAJUKUMU YA KAZI
 Kushauri juu ya Sera ya Ununuzi na Ugavi katika Wakala;
 Kushauri juu ya Mfumo wa Mtandao wa Ununuzi na Ugavi kwa kutumia kompyuta, “e-procurement”;
 Kutathmini taarifa ya vifaa vinavyotumika na Wakala ili kujua aina ya kasi ya vifaa husika kwa hatua zaidi;
 Kusimamia utayarishaji wa Mpango wa manunuzi wa Wakala;
 Kusimamia utayarishaji wa makisio ya vifaa vinavyohitajika katika Wakala;
 Kusimamia upimaji wa utendaji wa Maafisa Ugavi walio chini yake;
 Kumshauri Mtendaji Mkuu kuhusu namna bora kutekeleza majukumu yanayohusu ununuzi, utunzaji na ugavi katika Wakala;
1.1.3 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Shahada ya Ugavi na Shahada/Stashahada ya Uzamili katika fani za Biashara au Ugavi kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Bodi ya Taifa ya Usimamizi wa Vifaa, na uzoefu wa kazi usiopungua miaka kumi na mbili (12).
1.1.4 MSHAHARA
 Kwa kuzingatia ngazi za mishahara ya Serikali yaani WMAS 7 kwa mwezi
1.1.5 MCHUMI MKUU DARAJA LA I- NAFASI 1 (INARUDIWA)
1.1.6 MAJUKUMU YA KAZI
 Kuratibu na kuhuisha upangaji na udhibiti wa mipango ya Wakala;
 Kushiriki katika shughuli za kuandaa mipango, miongozo na nyaraka mbalimbali za Wakala;
 Kuchambua, kudhibiti na kuoanisha Bajeti ya Wakala kwa kushirikiana na Wizara mama;
 Kutayarisha taarifa za utekelezaji wa miradi ya maendeleo;
 Kutoa picha kamili ya uchumi wa Wakala na maendeleo yake kwa vipindi vya muda mfupi na kati;
 Kutayarisha miongozo ya maendeleo ya kila mwaka;
 Kutayarisha na kusimamia mifumo ya shughuli za mipango ya maendeleo;
 Kusimamia mwenendo wa kiuchumi wa Wakala na kutoa ushauri;
 Kusimamia upimaji wa utendaji wa watumishi walio chini yake;
1.1.7 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Shahada/Stashahada ya Uzamili (Masters/Postgraduate Diploma) ambao wamejiimarisha katika mojawapo ya fani zifuatazo Uchumi (Economics), Takwimu (Statistics), Sayansi ya Uchumi au Kilimo (Bsc. Agriculture Economics & Agri Business) kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.
 ujuzi wa kutumia kompyuta na uzoefu wa kazi ya uchambuzi wa masuala ya kiuchumi kwa muda usiopungua miaka kumi na mbili (12).
 Waombaji wenye Shahada ya Falsafa ya (Phd) katika fani husika au watakaokuwa wamechapisha makala zisizopungua sita (6) zinazohusiana na fani mbalimbali za uchumi watafikiriwa kwanza.
1.1.8 MSHAHARA
 Kwa kuzingatia ngazi za mishahara ya Serikali yaani WMAS 7 kwa mwezi.
2.0 FUNDI SANIFU MSAIDIZI (UPIMAJI ARDHI) - (ASSISTANT WATER WORKS TECHNICIAN GEOMETRIC) – NAFASI 24
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maji.
2.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufanya kazi kwa kuongozwa na chini ya uangalizi wa Fundi Sanifu aoyesajiliwa ili aweze;
 Kushirikiana na Wahandisi wa Maji na kuwaongoza walengwa katika kuchagua njia za kupitisha bomba kwa ajili ya miradi ya maji na usafi wa mazingira;
 Kupima hali ya kijiografia ya maeneo ya inayokusudiwa kujengwa au yenye miradi ya maji na usafi wa mazingira ili kuwezesha usanifu wa miundo mbinu miradi;
 Kupima uwekaji wa vifaa vya miundo mbinu kwenye ardhi wakati wa ujenzi wa miradi ya maji na usafi wa mazingira;
 Kunakili na kutunza taarifa za upimaji wa ardhi kwa ajili ya miundo mbinu ya miradi ya maji na usafi wa mazingira kwa namna inayokubalika kwa mchoraji wa ramani za usanifu wa miradi kufanya kazi yake kwa unadhifu;kuchora ramani za maeneo ya miradi ya maji na usafi wa mazingira kwa namna zote zinazokubalika kwa ajili ya kuwezesha usanifu wa miundo mbinu ya maji na usafi wa mazingira;
 Kumsaidia Fundi Sanifu katika kazi za upimaji ardhi.
2.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha nne waliohudhuria na kufaulu mafunzo ya mwaka mmoja kutoka Chuo cha Maji au Chuo chochote kinachitambuliwa na Serikali ambao wana Cheti cha ufundi Daraja III (Water Works Technician Geometric).
2.3 MSHAHARA
 Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS A kwa mwezi.
3.0 FUNDI SANIFU MSAIDIZI MITAMBO YA MAJI (PAMPU) – NAFASI 25
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maji.
3.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Atafanya kazi kwa kuongozwa na chini ya uangalizi wa Fundi Sanifu aliyesajiliwa ili aweze;
 Kufunga pampu na injini za aina mbalimbali za miradi ya maji na usafi wa mazingira;
 Kufanya usafi na ukaguzi wa pampu na injini za miradi ya maji na usafi wa mazingira kwa ajili ya kukidhi uendeshaji nadhifu, endelevu na kuzuia uharibifu;
 Kuhudumia uendeshaji wa pampu na injini za miradi ya maji;
 Kufanya matengenezo ya kawaida, ya vipindi na ya kuzuia uharibifu wa pampu na injini kwa kufuata miongozo ya uendeshaji na matengenezo na inapohitajika kwa dharura;
 Kunakiri, kutayarisha, kukusanya, kutunza na kuziwasilisha takwimu za uendeshaji na matengenezo ya pampu na injini za miradi ya maji;
 Kumsaidia Fundi Sanifu katika kazi za kiufundi.
3.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha nne waliohudhuria na kufaulu mafunzo ya mwaka mmoja kutoka Chuo cha Maji au Chuo chochote kinachitambuliwa na Serikali ambao wana Cheti cha ufundi Daraja III (Mitambo Ya Maji (Pampu).
3.3 MSHAHARA
 Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS A kwa mwezi.
4.0 FUNDI SANIFU MSAIDIZI MITAMBO YA MAJI (UMEME) – NAFASI 12
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maji.
4.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufanya kazi kwa kuongozwa na chini ya uangalizi wa Fundi sanifu aliyesajiliwa ili aweze;
 Kufunga mfumo wa umeme unaohitajika kwa ajili ya uendeshaji wa mitambo ya miradi ya maji na usafi wa mazingira;
 Kufunga mota na vifaa vingine vya umeme vya aina mbalimbali vya miradi ya maji na usafi wa mazingira;
 Kufanya usafi na ukaguzi wa mfumo wa umeme, mota na vifaa vingine umeme vya miradi ya maji na usafi wa mazingira kwa ajili ya kukidhi uendeshaji nadhifu wa pampu na kuzuia uharibifu;
 Kuendesha mitambo inayotumia umeme ya miradi ya maji na usafi wa mazingira;
 Kufanya matengenezo ya kawaida, ya vipindi na ya kuzuia uharibifu kwenye mfumo wa umeme, mota na vifaa vingine umeme kwa kufuata miongozo ya uendeshaji, na inapohitajika kwa dharura.
 Kunakili, kutayarisha, kukusanya, kutunza na kuziwasilisha takwimu za uendeshaji na matengenezo ya mitambo inayotumia umeme ya miradi ya maji na usafi wa mazingira;
 Kumsaidia Fundi Sanifu katika kazi za kiufundi.
4.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha nne waliohudhuria na kufaulu mafunzo ya mwaka mmoja kutoka Chuo cha Maji au Chuo chochote kinachitambuliwa na Serikali ambao wana Cheti cha ufundi Daraja III (Plants Technician Electrical).
4.3 MSHAHARA
 Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS A kwa mwezi.
5.0 MHANDISI DARAJA LA II (MAJI) – WATER RESOURCE ENGINEER –
NAFASI 2
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maji.
5.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kushughulikia upembuzi yakinifu, usanifu wa ujenzi, uendeshaji na matengenezo ya miundombinu midogo midogo ya usambazaji maji na kushiriki shughuli za upembuzi yakinifu, usanifu, ujenzi, uendeshaji na matengenezo ya miundombinu mikubwa ya ujenzi wa usambazaji maji na usafi wa mazingira.
 Kufanyia mapitio taarifa za upembuzi yakinifu na sanifu za ujenzi wa miundombinu ya miradi ya usambazaji maji na usafi wa mazingira.
 Kufanyia ukaguzi wa utekelezaji wa ujenzi, uendeshaji na utengenezaji wa miundombinu ya uzalishaji na usambazaji maji na usafi wa mazingira kwa ajili ya kupata ubora unaokusudiwa.
 Kushiriki katika kazi ya kupendekeza miradi na kupitia mapendekezo ya miradi (project proposal) ya usambazaji maji na usafi wa mazingira.
 Kufanya uchunguzi kuhusu uharibifu wa miundombinu au ajali zinazojitokeza wakati wa utekelezaji wa miradi ya maji na usafi wa mazingira.
 Kutayarisha bajeti ya utekelezaji wa shughuli za sekta za maji.
 Kusimamia kuratibu na kufuatilia utekelezaji wa ujenzi, uendeshaji na mategenezo ya miundombinu ya miradi ya maji na usafi wa mazingira.
 Kukusanya na kutayarisha taarifa mbalimbali za utekelezaji wa shughuli za sekta ya maji kwa ajili ya matumizi ya sekta na kwa ajili ya kujisajili katika bodi ya Wahandisi.
5.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Shahada/Stashahada ya juu ya uhandisi wa Maji (Water Resource Engineering) kutoka vyuo vikuu vinavyotambuliwa na Serikali.
5.3 MSHAHARA
 Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS E kwa mwezi.
6.0 MHANDISI DARAJA LA II (MAJI) – WATER RESOURCE WITH GIS ENGINEER – NAFASI 4
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maji.
6.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kushughulikia upembuzi yakinifu, usanifu wa ujenzi, uendeshaji na matengenezo ya miundombinu midogo midogo ya usambazaji maji na kushiriki shughuli za upembuzi yakinifu, usanifu, ujenzi, uendeshaji na matengenezo ya miundombinu mikubwa ya ujenzi wa usambazaji maji na usafi wa mazingira.
 Kufanyia mapitio taarifa za upembuzi yakinifu na sanifu za ujenzi wa miundombinu ya miradi ya usambazaji maji na usafi wa mazingira.
 Kufanyia ukaguzi wa utekelezaji wa ujenzi, uendeshaji na utengenezaji wa miundombinu ya uzalishaji na usambazaji maji na usafi wa mazingira kwa ajili ya kupata ubora unaokusudiwa.
 Kushiriki katika kazi ya kupendekeza miradi na kupitia mapendekezo ya miradi (project proposal) ya usambazaji maji na usafi wa mazingira.
 Kufanya uchunguzi kuhusu uharibifu wa miundombinu au ajali zinazojitokeza wakati wa utekelezaji wa miradi ya maji na usafi wa mazingira.
 Kutayarisha bajeti ya utekelezaji wa shughuli za sekta za maji.
 Kusimamia kuratibu na kufuatilia utekelezaji wa ujenzi, uendeshaji na mategenezo ya miundombinu ya miradi ya maji na usafi wa mazingira.
 Kukusanya na kutayarisha taarifa mbalimbali za utekelezaji wa shughuli za sekta ya maji kwa ajili ya matumizi ya sekta na kwa ajili ya kujisajili katika bodi ya Wahandisi.
6.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Shahada/Stashahada ya juu ya uhandisi wa Maji (Water Resource with GIS) kutoka vyuo vikuu vinavyotambuliwa na Serikali.
6.3 MSHAHARA
 Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS E kwa mwezi.
7.0 MHIFADHI WANYAMAPORI DARAJA LA II – NAFASI 31
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii.
7.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufanya doria ndani na nje ya maeneo ya hifadhi
 Kudhibiti vitendo vya ujangili nje na ndani ya hifadhi
 kusimamia uwindaji wa kitalii na utalii wa picha
 kulinda Nyara za Serikali
 Kusimamia usafirishaji wa wanyamapori na nyara nje na ndani ya Nchi
 Kusimamia matumizi ya magari ya doria
 Kukagua wanyamapori kwenye mashamba na mazizi ya wanyamapori na kutunza takwimu zao
 Kuratibu uingiaji wa wageni katika Mapori ya Akiba
 Kudhibiti moto katika hifadhi
 Kukusanya na kutunza vielelezo vya ushahidi na kutoa ushahidi Mahakamani
 Kukusanya takwimu za wanyama na mimea kwenye hifadhi
 Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa zinazoendana na taaluma yake
7.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha IV au kidato cha VI wenye Stashahada ya Uhifadhi Wanyamapori (Diploma in Wildlife Management) kutoka Chuo cha Usimamizi Wanyamapori Mweka au Chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali.
7.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi.
8.0 MHIFADHI MAMBO YA KALE II (CONSERVATORS OF ANTIQUITIES GRADE II) – NAFASI 4
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii.
8.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kushiriki katika kutunza na kuhifadhi mazingira ya vituo na maeneo ya Mambo ya Kale.
 Kushiriki katika kufanya kazi za ukarabati wa majengo
 Kushiriki katika kuboresha maeneo yenye umuhimu ya kihistoria.
 Kushiriki katika kufanya kazi za ufundi
 Kuratibu na kupokea wageni mbalimbali wanaotembelea Vituo vya Mambo ya Kale.
 Kushiriki katika kufanya utafiti na uhifadhi.
 Kushiriki kuandaa tathmini ya maeneo ambayo yamefanyiwa utafiti na uhifadhi.
 Kuratibu ushauri wa kurekebisha vipengele vya Sheria ya Mambo ya Kale.
 Kuendesha mafunzo ya Elimu ya Jamii kuhusu masuala ya utafiti na uhifadhi kwa njia ya semina, warsha na vipindi vya radio.
 Kushiriki katika kuandaa vipindi vya TV na Radio
 Kushiriki katika kuandaa kazi za maabara.
 Kushiriki katika kuandaa kumbukumbu za mambo ya kale.
8.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Shahada/stashahada ya juu ya Sayansi ya Jamii au Sayansi ya Asili, waliojiimarisha (major) katika mojawapo ya michepuo ya Jiologia, elimu ya viumbe, Akiolojia, Anthropolojia, Jiografia, Historia, Paleontolojia au Ethnolojia kutoka Vyuo vinavyotambulika na Serikali.
8.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali ngazi ya Mshahara TGS.D kwa mwezi.
9.0 AFISA ELIMU DARAJA LA II (EDUCATION OFFICER GRADE II) – KISWAHILI (NAFASI 16)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto.Walimu hawa watafanya kazi ya kufundisha katika vyuo vya maendeleo ya wananchi vilivyopo katika mikoa yote ya Tanzania Bara.
9.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la Kiswahili katika vyuo vya maendeleo ya wananchi.
 Kuandaa maazimio ya kazi, maandalio ya masomo, zana za kufundishia /kujifunzia, mazoezi ya wanafunzi na majaribio.
 Kutunga, kusimamia na kusahihisha mitihani kwa lengo la kutathmini maendeleo ya wanachuo.
 Kuandaa mazoezi ya kazi kwa wanachuo na kusahihisha.
 Kuandaa taarifa za kitaaluma na kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanachuo na kuwasilisha katika mamlaka husika.
 Kufanya tafiti mbalimbali za kielimu.
 Kushika zamu na kutoa taarifa kwa uongozi wa chuo.
 Kutunza na kudhibiti matumizi ya vifaa katika sehemu aliyokabidhiwa.
 Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa ngazi za juu kuhusu masuala mbalimbali kulingana na majukumu aliyopewa.
 Kutoa ushauri nasaha na kuwalea wanachuo kwa kuwaandaa kiakili,kimwili,kitabia na kimwenendo ili waweze kujua wajibu wao kwa jamii
 Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Chuo.
9.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Shahada ya kwanza kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali waliosoma somo la Kiswahili. Aidha kipaumbele ni walimu wenye Shahada ya Elimu ya Watu Wazima katika somo tajwa hapo juu.
 Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta.
9.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGTS D kwa mwezi.
10.0 AFISA ELIMU DARAJA LA II (EDUCATION OFFICER GRADE II) – KIINGEREZA (NAFASI 14)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto.Walimu hawa watafanya kazi ya kufundisha katika vyuo vya maendeleo ya wananchi vilivyopo katika mikoa yote ya Tanzania Bara.
10.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la Kiingereza katika vyuo vya Maendeleo ya wananchi.
 Kuandaa maazimio ya kazi, maandalio ya masomo, zana za kufundishia /kujifunzia, mazoezi ya wanafunzi na majaribio.
 Kutunga, kusimamia na kusahihisha mitihani kwa lengo la kutathmini maendeleo ya wanachuo.
 Kuandaa mazoezi ya kazi kwa wanachuo na kusahihisha.
 Kuandaa taarifa za kitaaluma na kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanachuo na kuwasilisha katika mamlaka husika.
 Kufanya tafiti mbalimbali za kielimu.
 Kushika zamu na kutoa taarifa kwa uongozi wa chuo.
 Kutunza na kudhibiti matumizi ya vifaa katika sehemu aliyokabidhiwa.
 Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa ngazi za juu kuhusu masuala mbalimbali kulingana na majukumu aliyopewa.
 Kutoa ushauri nasaha na kuwalea wanachuo kwa kuwaandaa kiakili,kimwili,kitabia na kimwenendo ili waweze kujua wajibu wao kwa jamii
 Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Chuo.
10.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Shahada ya kwanza kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali waliosoma somo la Kiingereza.Aidha kipaumbele ni walimu wenye shahada ya Elimu ya Watu Wazima katika somo tajwa hapo juu.
 Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta.
10.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGTS D kwa mwezi.
11.0 AFISA ELIMU DARAJA LA II (EDUCATION OFFICER GRADE II) – URAIA (CIVIC EDUCATION) (NAFASI 30)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto.Walimu hawa watafanya kazi ya kufundisha katika vyuo vya maendeleo ya wananchi vilivyopo katika mikoa yote ya Tanzania Bara.
11.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la uraia katika vyuo vya Maendeleo ya Wananchi.
 Kuandaa maazimio ya kazi, maandalio ya masomo, zana za kufundishia /kujifunzia, mazoezi ya wanafunzi na majaribio.
 Kutunga, kusimamia na kusahihisha mitihani kwa lengo la kutathmini maendeleo ya wanachuo.
 Kuandaa mazoezi ya kazi kwa wanachuo na kusahihisha.
 Kuandaa taarifa za kitaaluma na kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanachuo na kuwasilisha katika mamlaka husika.
 Kufanya tafiti mbalimbali za kielimu.
 Kushika zamu na kutoa taarifa kwa uongozi wa chuo.
 Kutunza na kudhibiti matumizi ya vifaa katika sehemu aliyokabidhiwa.
 Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa ngazi za juu kuhusu masuala mbalimbali kulingana na majukumu aliyopewa.
 Kutoa ushauri nasaha na kuwalea wanachuo kwa kuwaandaa kiakili,kimwili,kitabia na kimwenendo ili waweze kujua wajibu wao kwa jamii
 Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Chuo.
11.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Shahada ya kwanza kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali waliosomea Development Studies au Political Science. Aidha kipaumbele ni walimu wenye shahada ya Elimu ya Watu Wazima katika somo tajwa hapo juu.
 Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta
11.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGTS D kwa mwezi.
12.0 AFISA ELIMU DARAJA LA II (EDUCATION OFFICER GRADE II) –BACHELOR OF EDUCATION IN COMMERCE)- (NAFASI 30)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto.Walimu hawa watafanya kazi ya kufundisha katika vyuo vya maendeleo ya jamii na Maendeleo ya Wananchi vilivyopo katika mikoa yote ya Tanzania Bara.
12.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha masomo ya Hesabu za biashara na Ujasiriamali katika vyuo vya Maendeleo ya Wananchi.
 Kuandaa maazimio ya kazi, maandalio ya masomo, zana za kufundishia /kujifunzia, mazoezi ya wanafunzi na majaribio.
 Kutunga, kusimamia na kusahihisha mitihani kwa lengo la kutathmini maendeleo ya wanachuo.
 Kuandaa mazoezi ya kazi kwa wanachuo na kusahihisha.
 Kuandaa taarifa za kitaaluma na kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanachuo na kuwasilisha katika mamlaka husika.
 Kufanya tafiti mbalimbali za kielimu.
 Kushika zamu na kutoa taarifa kwa uongozi wa chuo.
 Kutunza na kudhibiti matumizi ya vifaa katika sehemu aliyokabidhiwa.
 Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa ngazi za juu kuhusu masuala mbalimbali kulingana na majukumu aliyopewa.
 Kutoa ushauri nasaha na kuwalea wanachuo kwa kuwaandaa kiakili,kimwili,kitabia na kimwenendo ili waweze kujua wajibu wao kwa jamii
 Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Chuo
12.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Shahada ya kwanza kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali waliosomea Elimu ya Biashara na ualimu (Bachelor Of Education in Commerce).
 Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta
12.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGTS D kwa mwezi.
13.0 AFISA ELIMU DARAJA LA II (EDUCATION OFFICER GRADE II) –HISABATI (MATHEMATICS) (NAFASI 15)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto.Walimu hawa watafanya kazi ya kufundisha katika vyuo vya maendeleo ya jamii na Maendeleo ya Wananchi vilivyopo katika mikoa yote ya Tanzania Bara.
13.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la Hesabu katika vyuo 25 vya Maendeleo ya Wananchi vinavyofundisha mafunzo ya Ufundi Stadi.
 Kuandaa maazimio ya kazi, maandalio ya masomo, zana za kufundishia /kujifunzia, mazoezi ya wanafunzi na majaribio.
 Kutunga, kusimamia na kusahihisha mitihani kwa lengo la kutathmini maendeleo ya wanachuo.
 Kuandaa mazoezi ya kazi kwa wanachuo na kusahihisha.
 Kuandaa taarifa za kitaaluma na kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanachuo na kuwasilisha katika mamlaka husika.
 Kufanya tafiti mbalimbali za kielimu.
 Kushika zamu na kutoa taarifa kwa uongozi wa chuo.
 Kutunza na kudhibiti matumizi ya vifaa katika sehemu aliyokabidhiwa.
 Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa ngazi za juu kuhusu masuala mbalimbali kulingana na majukumu aliyopewa.
 Kutoa ushauri nasaha na kuwalea wanachuo kwa kuwaandaa kiakili,kimwili,kitabia na kimwenendo ili waweze kujua wajibu wao kwa jamii
 Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Chuo
13.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Shahada ya kwanza kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali waliosomea Hisabati na Ualimu (Bachelor of Education in Mathematics).
 Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta
13.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGTS D kwa mwezi.
14.0 AFISA ELIMU DARAJA LA II (EDUCATION OFFICER GRADE II) –KEMIA (CHEMISTRY) (NAFASI 5)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto.Walimu hawa watafanya kazi ya kufundisha katika vyuo vya maendeleo ya jamii na Maendeleo ya Wananchi vilivyopo katika mikoa yote ya Tanzania Bara.
14.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la Kemia katika vyuo 25 vya Maendeleo ya Wananchi vinavyofundisha mafunzo ya Ufundi stadi.
 Kuandaa maazimio ya kazi, maandalio ya masomo, zana za kufundishia /kujifunzia, mazoezi ya wanafunzi na majaribio.
 Kutunga, kusimamia na kusahihisha mitihani kwa lengo la kutathmini maendeleo ya wanachuo.
 Kuandaa mazoezi ya kazi kwa wanachuo na kusahihisha.
 Kuandaa taarifa za kitaaluma na kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanachuo na kuwasilisha katika mamlaka husika.
 Kufanya tafiti mbalimbali za kielimu.
 Kushika zamu na kutoa taarifa kwa uongozi wa chuo.
 Kutunza na kudhibiti matumizi ya vifaa katika sehemu aliyokabidhiwa.
 Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa ngazi za juu kuhusu masuala mbalimbali kulingana na majukumu aliyopewa.
 Kutoa ushauri nasaha na kuwalea wanachuo kwa kuwaandaa kiakili,kimwili,kitabia na kimwenendo ili waweze kujua wajibu wao kwa jamii
 Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Chuo.
14.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Shahada ya kwanza kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali katika somo la Kemia (Chemistry).
 Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta
14.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGTS D kwa mwezi.
15.0 AFISA ELIMU DARAJA LA II (EDUCATION OFFICER GRADE II) –FIZIKIA (PHYSICS) (NAFASI 14)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto.Walimu hawa watafanya kazi ya kufundisha katika vyuo vya maendeleo ya jamii na Maendeleo ya Wananchi vilivyopo katika mikoa yote ya Tanzania Bara.
15.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la Fizikia katika vyuo vyuo 25 vya Maendeleo ya Wananchi vinavyofundisha mafunzo ya Ufundi Sanifu
 Kuandaa maazimio ya kazi, maandalio ya masomo, zana za kufundishia /kujifunzia, mazoezi ya wanafunzi na majaribio.
 Kutunga, kusimamia na kusahihisha mitihani kwa lengo la kutathmini maendeleo ya wanachuo.
 Kuandaa mazoezi ya kazi kwa wanachuo na kusahihisha.
 Kuandaa taarifa za kitaaluma na kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanachuo na kuwasilisha katika mamlaka husika.
 Kufanya tafiti mbalimbali za kielimu.
 Kushika zamu na kutoa taarifa kwa uongozi wa chuo.
 Kutunza na kudhibiti matumizi ya vifaa katika sehemu aliyokabidhiwa.
 Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa ngazi za juu kuhusu masuala mbalimbali kulingana na majukumu aliyopewa.
 Kutoa ushauri nasaha na kuwalea wanachuo kwa kuwaandaa kiakili,kimwili,kitabia na kimwenendo ili waweze kujua wajibu wao kwa jamii
 Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Chuo
15.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Shahada ya kwanza kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali katika somo la Fizikia (Physics).
 Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta
15.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGTS D kwa mwezi.
16.0 AFISA ELIMU DARAJA LA II (EDUCATION OFFICER GRADE II) –SAYANSI KIMU(DOMESTIC SCIENCE) (NAFASI 30)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto.Walimu hawa watafanya kazi ya kufundisha katika vyuo vya maendeleo ya jamii na Maendeleo ya Wananchi vilivyopo katika mikoa yote ya Tanzania Bara.
16.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la upishi na lishe,hotel management, uhifadhi wa vyakula,uzalishaji vyakula na vinywaji katika, vyuo vya Maendeleo ya Wananchi
 Kuandaa maazimio ya kazi, maandalio ya masomo, zana za kufundishia /kujifunzia, mazoezi ya wanafunzi na majaribio.
 Kutunga, kusimamia na kusahihisha mitihani kwa lengo la kutathmini maendeleo ya wanachuo.
 Kuandaa mazoezi ya kazi kwa wanachuo na kusahihisha.
 Kuandaa taarifa za kitaaluma na kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanachuo na kuwasilisha katika mamlaka husika.
 Kufanya tafiti mbalimbali za kielimu.
 Kushika zamu na kutoa taarifa kwa uongozi wa chuo.
 Kutunza na kudhibiti matumizi ya vifaa katika sehemu aliyokabidhiwa.
 Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa ngazi za juu kuhusu masuala mbalimbali kulingana na majukumu aliyopewa.
 Kutoa ushauri nasaha na kuwalea wanachuo kwa kuwaandaa kiakili,kimwili,kitabia na kimwenendo ili waweze kujua wajibu wao kwa jamii
 Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Chuo
16.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Shahada ya kwanza kutoka chuo Kikuu cha Sokoine na vyuo Vikuu vingine vinavyotambuliwa na Serikali waliosomea Maarifa ya nyumbani (Home Economics/Domestic Science)
 Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta.
16.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGTS D kwa mwezi.
17.0 MWANASHERIA DARAJA LA II (LAWYER GRADE II) –SHERIA (LAW) (NAFASI 8)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto.Walimu hawa watafanya kazi ya kufundisha katika vyuo vya maendeleo ya jamii na Maendeleo ya Wananchi vilivyopo katika mikoa yote ya Tanzania Bara.
17.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la sheria katika vyuo vya Maendeleo ya Jamii.
 Kuandaa maazimio ya kazi, maandalio ya masomo, zana za kufundishia /kujifunzia, mazoezi ya wanafunzi na majaribio.
 Kutunga, kusimamia na kusahihisha mitihani kwa lengo la kutathmini maendeleo ya wanachuo.
 Kuandaa mazoezi ya kazi kwa wanachuo na kusahihisha.
 Kuandaa taarifa za kitaaluma na kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanachuo na kuwasilisha katika mamlaka husika.
 Kufanya tafiti mbalimbali za kielimu.
 Kushika zamu na kutoa taarifa kwa uongozi wa chuo.
 Kutunza na kudhibiti matumizi ya vifaa katika sehemu aliyokabidhiwa.
 Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa ngazi za juu kuhusu masuala mbalimbali kulingana na majukumu aliyopewa.
 Kutoa ushauri nasaha na kuwalea wanachuo kwa kuwaandaa kiakili,kimwili,kitabia na kimwenendo ili waweze kujua wajibu wao kwa jamii
 Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Chuo
17.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Shahada ya kwanza kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali waliosomea Sheria (Law)
 Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta
17.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS E kwa mwezi.
18.0 MWALIMU DARAJA LA III (TEACHER GRADE III) –UFUNDI CHUMA (WELDING AND METAL FABRICATION) (NAFASI 2)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto.Walimu hawa watafanya kazi ya kufundisha Masomo ya Ufundi katika vyuo 55 vya Maendeleo ya Wananchi vilivyopo katika mikoa yote ya Tanzania Bara.
18.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la uungaji vyuma katika vyuo vya Maendeleo ya Wananchi.
 Kuandaa maazimio ya kazi, maandalio ya masomo, zana za kufundishia /kujifunzia, mazoezi ya wanafunzi na majaribio.
 Kutunga, kusimamia na kusahihisha mitihani kwa lengo la kutathmini maendeleo ya wanachuo.
 Kuandaa mazoezi ya kazi kwa wanachuo na kusahihisha.
 Kuandaa taarifa za kitaaluma na kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanachuo na kuwasilisha katika mamlaka husika.
 Kufanya tafiti mbalimbali za kielimu.
 Kushika zamu na kutoa taarifa kwa uongozi wa chuo.
 Kutunza na kudhibiti matumizi ya vifaa katika sehemu aliyokabidhiwa.
 Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa ngazi za juu kuhusu masuala mbalimbali kulingana na majukumu aliyopewa.
 Kutoa ushauri nasaha na kuwalea wanachuo kwa kuwaandaa kiakili,kimwili,kitabia na kimwenendo ili waweze kujua wajibu wao kwa jamii
 Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Chuo.
18.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye cheti cha Mtihani wa Taifa wa kidato cha Nne/sita na mafunzo ya ualimu miaka miwili (2) na kuapata cheti cha Ualimu daraja la IIIA katika fani ya uungaji vyuma (Welding And Metal Fabrication) na kusomea ualimu kwa miaka miwili.
 Aidha kipaumbele ni kwa walimu waliohitimu katika vyuo Ualimu vya Klerruu, Mtwara Ufundi na Dakawa na vyuo vingine vinavyotambulika na serikali.
18.3 10.2 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGTS B kwa mwezi.
19.0 MWALIMU DARAJA LA III (TEACHER GRADE III) –USHONAJI NA UFUMAJI(KNITTING AND EMBROIDERY) (NAFASI 3)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto.Walimu hawa watafanya kazi ya kufundisha Masomo ya Ufundi katika vyuo vya maendeleo ya Wananchi vilivyopo katika mikoa yote ya Tanzania Bara.
19.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la ushonaji na ufumaji katika vyuo vya Maendeleo ya Wananchi.
 Kuandaa maazimio ya kazi, maandalio ya masomo, zana za kufundishia /kujifunzia, mazoezi ya wanafunzi na majaribio.
 Kutunga, kusimamia na kusahihisha mitihani kwa lengo la kutathmini maendeleo ya wanachuo.
 Kuandaa mazoezi ya kazi kwa wanachuo na kusahihisha.
 Kuandaa taarifa za kitaaluma na kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanachuo na kuwasilisha katika mamlaka husika.
 Kufanya tafiti mbalimbali za kielimu.
 Kushika zamu na kutoa taarifa kwa uongozi wa chuo.
 Kutunza na kudhibiti matumizi ya vifaa katika sehemu aliyokabidhiwa.
 Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa ngazi za juu kuhusu masuala mbalimbali kulingana na majukumu aliyopewa.
 Kutoa ushauri nasaha na kuwalea wanachuo kwa kuwaandaa kiakili,kimwili,kitabia na kimwenendo ili waweze kujua wajibu wao kwa jamii
 Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Chuo.
19.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye cheti cha Mtihani wa Taifa wa kidato cha Nne/sita na mafunzo ya ualimu miaka miwili (2) na kuapata cheti cha Ualimu daraja la IIIA katika Ushonaji na ufumaji (Knitting and Embroidery).
 Aidha kipaumbele ni kwa walimu waliohitimu katika vyuo Ualimu vya Klerruu, Mtwara Ufundi na Dakawa na vyuo vingine vinavyotambulika na serikali.
19.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGTS B kwa mwezi.
20.0 MWALIMU DARAJA LA III (TEACHER GRADE III) –UPISHI (COOKERY) (NAFASI 3)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto.Walimu hawa watafanya kazi ya kufundisha Masomo ya Ufundi katika vyuo vya maendeleo ya Wananchi vilivyopo katika mikoa yote ya Tanzania Bara.
20.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la Upishi katika vyuo vya Maendeleo ya Wananchi.
 Kuandaa maazimio ya kazi, maandalio ya masomo, zana za kufundishia /kujifunzia, mazoezi ya wanafunzi na majaribio.
 Kutunga, kusimamia na kusahihisha mitihani kwa lengo la kutathmini maendeleo ya wanachuo.
 Kuandaa mazoezi ya kazi kwa wanachuo na kusahihisha.
 Kuandaa taarifa za kitaaluma na kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanachuo na kuwasilisha katika mamlaka husika.
 Kufanya tafiti mbalimbali za kielimu.
 Kushika zamu na kutoa taarifa kwa uongozi wa chuo.
 Kutunza na kudhibiti matumizi ya vifaa katika sehemu aliyokabidhiwa.
 Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa ngazi za juu kuhusu masuala mbalimbali kulingana na majukumu aliyopewa.
 Kutoa ushauri nasaha na kuwalea wanachuo kwa kuwaandaa kiakili,kimwili,kitabia na kimwenendo ili waweze kujua wajibu wao kwa jamii
 Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Chuo.
20.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye cheti cha Mtihani wa Taifa wa kidato cha Nne/sita na mafunzo ya ualimu miaka miwili (2) na kuapata cheti cha Ualimu daraja la IIIA katika Upishi (Cookery).
 Aidha kipaumbele ni kwa walimu waliohitimu katika vyuo Ualimu vya Klerruu, Mtwara Ufundi na Dakawa na vyuo vingine vinavyotambulika na serikali.
20.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGTS B kwa mwezi.
21.0 MWALIMU DARAJA LA III (TEACHER GRADE III) –UFUNDI UJENZI (CIVIL) (NAFASI 3)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto.Walimu hawa watafanya kazi ya kufundisha Masomo ya Ufundi katika vyuo vya maendeleo ya Wananchi vilivyopo katika mikoa yote ya Tanzania Bara.
21.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la ujenzi katika vyuo vya Maendeleo ya Wananchi.
 Kuandaa maazimio ya kazi, maandalio ya masomo, zana za kufundishia /kujifunzia, mazoezi ya wanafunzi na majaribio.
 Kutunga, kusimamia na kusahihisha mitihani kwa lengo la kutathmini maendeleo ya wanachuo.
 Kuandaa mazoezi ya kazi kwa wanachuo na kusahihisha.
 Kuandaa taarifa za kitaaluma na kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanachuo na kuwasilisha katika mamlaka husika.
 Kufanya tafiti mbalimbali za kielimu.
 Kushika zamu na kutoa taarifa kwa uongozi wa chuo.
 Kutunza na kudhibiti matumizi ya vifaa katika sehemu aliyokabidhiwa.
 Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa ngazi za juu kuhusu masuala mbalimbali kulingana na majukumu aliyopewa.
 Kutoa ushauri nasaha na kuwalea wanachuo kwa kuwaandaa kiakili,kimwili,kitabia na kimwenendo ili waweze kujua wajibu wao kwa jamii
 Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Chuo.
21.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye cheti cha Mtihani wa Taifa wa kidato cha Nne/sita ambao walisomea somo la ujenzi na mafunzo ya ualimu miaka miwili (2) na kupata cheti cha Ualimu daraja la IIIA katika fani ya Ujenzi (Civil).
 Aidha kipaumbele ni kwa walimu waliohitimu katika vyuo Ualimu vya Klerruu, Mtwara Ufundi na Dakawa na vyuo vingine vinavyotambulika na serikali
21.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGTS B kwa mwezi.
22.0 TABIBU II (CLINICAL OFFICERS) – (NAFASI 7)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto. Tabibu hawa watafanya kazi ya kutoa huduma ya kwanza na utabibu kwa wanachuo na jamii inayokizunguka chuo katika vyuo vya maendeleo ya Wananchi vilivyopo katika mikoa yote ya Tanzania Bara.
22.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kazi zote zinazofanywa na Tabibu Msaidizi
 Kutambua na kutibu magonjwa ya kawaida kwa wanachuo na jamii inayokizunguka chuo.
 Kutoa ushauri wa kiafya kwa wanachuo na jamii inayokizunguka chuo.
 Kusimamia utendaji wa watumishi walio chini yake na kufanya upasuaji mdogo
 Kushiriki katika kupanga na kutekeleza huduma za Afya msingi
 Kushauri na kuhamasisha wanachuo kuchangia huduma za afya na Mfuko wa Afya ya jamii.
 Kufundisha somo la afya ya jamii chuoni.
22.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita wenye Stashahada ya Tabibu ya miaka mwitatu kutoka chuo kinachotambuliwa na serikali.
22.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGHS B kwa mwezi.
23.0 II (NURSE II) – (NAFASI 2)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto. Wahudumu wa afya (Nurse) hawa watafanya kazi ya kutoa huduma ya kwanza na kwa wanachuo na jamii inayokizunguka chuo katika vyuo vya maendeleo ya Wananchi vilivyopo katika mikoa yote ya Tanzania Bara
23.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kutoa huduma ya kwanza kwa wanachuo na jamii inayokizunguka chuo.
 Kuangalia afya za wanachuo na jamii inayokizunguka chuo na kutoa ushauri kwa uongozi wa chuo.
 Kutoa elimu ya afya ya jamii kwa wanachuo na jamii inayokizunguka chuo.
 Kushirikiana na tabibu katika kutekeleza majukumu yake.
23.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita wenye stashahada ya Uuguzi ya miaka mwitatu kutoka chuo cha afya kinachotambuliwa na serikali.
23.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGHS A kwa mwezi.
24.0 MKUFUNZI DARAJA LA II –MHANDISI MAJI (WATER TECHNOLOGY) – (NAFASI 1)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto. Mhandisi huyu atafanya kazi ya kufundisha somo la Uhandisi wa Maji katika vyuo vya maendeleo ya Jamii Tanzania Bara
24.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la Uhandisi maji katika vyuo vya maendeleo ya jamii.
 Kutayarisha mpango wa kazi wa Mafunzo
 Kupima Maendeleo ya Wanachuo katika nadharia na vitendo
 Kutunza vifaa vya kujifunzia na kufundishia
 Kufanya na kutoa taarifa za Utafiti
 Kutoa Ushauri wa kitaalam kuhusu somo la uhandisi maji.
 Kutunga na kusahihisha Mitihani ya wanachuo.
 Kufanya Utafiti utakosaidia kutoa majibu kwa matatizo/changamoto mbaimbali katika jamii inayoizunguka chuo
 Kutoa Ushauri juu ya kuboresha Taaluma chuoni.
24.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha sita waliofuzu Mafunzo ya Shahada/ stashahada ya juu katika fani ya Uhandisi Maji (Water Technology) kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.
24.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS E kwa mwezi.
25.0 MKUFUNZI DARAJA LA II –MHANDISI MITAMBO (METAL TECHNOLOGY) – (NAFASI 2)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto. Wahandisi hawa watafanya kazi ya kufundisha somo la Ufundi Mitambo katika vyuo vya maendeleo ya Jamii Tanzania Bara
25.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la ufundi mitambo katika vyuo vya Maendeleo ya Jamii.
 Kutayarisha mpango wa kazi wa Mafunzo
 Kupima Maendeleo ya Wanachuo katika nadharia na vitendo
 Kutunza vifaa vya kujifunzia na kufundishia
 Kufanya na kutoa taarifa za Utafiti
 Kutoa ushauri wa kitaalam kuhusu somo la uhandisi maji.
 Kutunga na kusahihisha Mitihani ya wanachuo.
 Kufanya utafiti utakosaidia kutoa majibu kwa matatizo/changamoto mbaimbali
 katika jamii inayoizunguka chuo
 Kutoa ushauri juu ya kuboresha Taaluma chuoni
25.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha sita waliofuzu Mafunzo ya Shahada/ stashahada ya juu katika fani ya Uhandisi Mitambo (Metal Technology) kutoka katika vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.
25.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS E kwa mwezi.
26.0 MKUFUNZI DARAJA LA II- UUNGA VYUMA (MECHANICAL ENGINEER)-(NAFASI 24)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto. Wahandisi hawa watafanya kazi ya kufundisha somo la Uungaji vyuma, computer Application na technical drawing katika vyuo vya maendeleo ya Wananchi Tanzania Bara
26.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la uungaji vyuo, computer application na Technical drawing katika vyuo vyuo vya maendeleo ya wananchi.
 Kutayarisha mpango wa kazi wa Mafunzo
 Kupima Maendeleo ya Wanachuo katika nadharia na vitendo
 Kutunza vifaa vya kufundishia
 Kufanya na kutoa taarifa za Utafiti
 Kutoa Ushauri wa kitaalam
 Kuandaaa kanuni na taratibu za kusimamia Mitihani chuoni
 Kutunga na kusahihisha Mitihani
 Kufanya Utafiti utakaosaidia kutoa majibu kwa matatizo/changamoto mbaimbali katika jamii inayoizunguka chuo
 Kutoa ushauri juu ya kuboresha taaluma chuoni na kuendeleza Mafunzo nje ya chuo
26.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu Mafunzo ya Shahada/ stashahada ya juu katika fani ya Uunga vyuma, ufundi bomba, computer application and technical (Mechanical Engeneering) kutoka katika vyuo vinavyotambuliwa na Serikali
26.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D/E kwa mwezi.
27.0 MKUFUNZI DARAJA LA II- MHANDISI UJENZI (CIVIL ENGINEER)-(NAFASI 25)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto. Wahandisi hawa watafanya kazi ya kufundisha somo la Ujenzi, computer Application na technical drawing katika vyuo (24) vya maendeleo ya Wananchi na chuo cha Maendeleo ya Jamii Missungwi
27.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la uungaji vyuo, computer application na Technical drawing katika vyuo vyuo vya maendeleo ya wananchi.
 Kutayarisha mpango wa kazi wa Mafunzo
 Kupima Maendeleo ya Wanachuo katika nadharia na vitendo
 Kutunza vifaa vya kufundishia
 Kufanya na kutoa taarifa za Utafiti
 Kutoa Ushauri wa kitaalam
 Kuandaaa kanuni na taratibu za kusimamia Mitihani chuoni
 Kutunga na kusahihisha Mitihani
 Kufanya Utafiti utakaosaidia kutoa majibu kwa matatizo/changamoto mbaimbali katika jamii inayoizunguka chuo
 Kutoa ushauri juu ya kuboresha taaluma chuoni na kuendeleza Mafunzo nje ya chuo
27.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu Mafunzo ya Shahada/ stashahada ya juu katika fani ya uhandisi majengo(Civil Engeneering), Uunga vyuma, computer application and technical drawing kutoka katika vyuo vinavyotambuliwa na Serikali
27.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D/E kwa mwezi.
28.0 MKUFUNZI DARAJA LA II- COMPUTER SCIENCE (NAFASI 5)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto. Wahandisi hawa watafanya kazi ya kufundisha somo la computer na electronics (Computer Application) katika vyuo vya maendeleo ya WananchiTanzania Bara
28.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la computer na electronics katika vyuo vya maendeleo ya wananchi.
 Kutayarisha mpango wa kazi wa Mafunzo
 Kupima Maendeleo ya Wanachuo katika nadharia na vitendo
 Kutunza vifaa vya kufundishia
 Kufanya na kutoa taarifa za Utafiti
 Kutoa Ushauri wa kitaalam
 Kuandaaa kanuni na taratibu za kusimamia Mitihani chuoni
 Kutunga na kusahihisha Mitihani
 Kufanya Utafiti utakosaidia kutoa majibu kwa matatizo/hangamoto mbaimbali katika jamii inayoizunguka chuo
 Kutoa Ushauri juu ya kuboresha Taaluma chuoni na kuendeleza Mafunzo nje ya chuo
28.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu Mafunzo ya Shahada/ stashahada ya juu katika fani ya computer science kutoka katika vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.
28.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.
29.0 MKUFUNZI DARAJA LA II- ELECTRICAL ENGINEER - (NAFASI 20)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Wakufunzi hawa watafanya kazi ya kufundisha somo la Umeme wa majumbani (Electrical installation), computer application na technical drawing katika vyuo vya maendeleo ya Jamii Tanzania Bara
29.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la umeme wa majumbani, computer application na technical drawing katika vyuo vya maendeleo ya wananchi.
 Kutayarisha mpango wa kazi wa Mafunzo
 Kupima Maendeleo ya Wanachuo katika nadharia na vitendo
 Kutunza vifaa vya kufundishia
 Kufanya na kutoa taarifa za Utafiti
 Kutoa Ushauri wa kitaalam
 Kuandaaa kanuni na taratibu za kusimamia Mitihani chuoni
 Kutunga na kusahihisha Mitihani
 Kufanya Utafiti utakosaidia kutoa majibu kwa matatizo/hangamoto mbaimbali katika jamii inayoizunguka chuo
 Kutoa Ushauri juu ya kuboresha Taaluma chuoni na kuendeleza Mafunzo nje ya chuo
29.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu Mafunzo ya Shahada/ stashahada ya juu katika fani ya Electrical Engineering kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.
29.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS E kwa mwezi.
30.0 MKUFUNZI DARAJA LA II- KILIMO (AGRICULTURAL OFFICER )- (NAFASI 10)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Wakufunzi hawa watafanya kazi ya kufundisha somo la kilimo (Agriculture) katika vyuo vya maendeleo ya wananchi Tanzania Bara
30.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la kilimo katika vyuo vya maendeleo ya wananchi.
 Kutayarisha mpango wa kazi wa Mafunzo
 Kupima Maendeleo ya Wanachuo katika nadharia na vitendo
 Kutunza vifaa vya kufundishia
 Kufanya na kutoa taarifa za Utafiti
 Kutoa Ushauri wa kitaalam
 Kuandaaa kanuni na taratibu za kusimamia Mitihani chuoni
 Kutunga na kusahihisha Mitihani
 Kufanya Utafiti utakosaidia kutoa majibu kwa matatizo/hangamoto mbalimbali katika jamii inayoizunguka chuo
 Kutoa Ushauri juu ya kuboresha Taaluma chuoni na kuendeleza Mafunzo nje ya chuo
30.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu Mafunzo ya Shahada/ stashahada ya juu katika somo la kilimo kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.
30.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.
31.0 MKUFUNZI MSAIDIZI DARAJA LA II–HOME ECONOMICS/ DOMESTIC SCIENCE
(NAFASI 9)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Wakufunzi wasaidizi hawa watafanya kazi ya kufundisha somo la ushonaji, ufumaji, kudarizi, upishi na lishe katika vyuo vya maendeleo ya wananchi Tanzania Bara
31.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha masomo ya ushonaji, ufumaji, kudarizi na upishi na lishe katika vyuo vya maendeleo ya wananchi.
 Kutayarisha mpango wa kazi wa Mafunzo
 Kupima Maendeleo ya Wanachuo katika nadharia na vitendo
 Kutunza vifaa vya kufundishia
 Kufanya na kutoa taarifa za Utafiti
 Kutoa Ushauri wa kitaalam
 Kuandaaa kanuni na taratibu za kusimamia Mitihani chuoni
 Kutunga na kusahihisha Mitihani
 Kufanya Utafiti utakosaidia kutoa majibu kwa matatizo/hangamoto mbalimbali katika jamii inayoizunguka chuo
 Kutoa Ushauri juu ya kuboresha Taaluma chuoni na kuendeleza Mafunzo nje ya chuo
31.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu mafunzo ya stashahada ya ufundi katika fani za ushonaji, ufumaji, kudarizi, upishi na lishe kutoka vyuo vya ufundi vinanvyotambuliwa na Serikali.
31.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi.
32.0 MKUFUNZI MSAIDIZI DARAJA LA II – KILIMO - (NAFASI 8)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Wakufunzi wasaidizi hawa watafanya kazi ya kufundisha somo la Kilimo katika vyuo vya maendeleo ya wananchi Tanzania Bara
32.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la kilimo na mifugo katika vyuo vya maendeleo ya wananchi.
 Kutayarisha mpango wa kazi wa Mafunzo
 Kupima Maendeleo ya Wanachuo katika nadharia na vitendo
 Kutunza vifaa vya kufundishia
 Kufanya na kutoa taarifa za Utafiti
 Kutoa Ushauri wa kitaalam
 Kuandaaa kanuni na taratibu za kusimamia Mitihani chuoni
 Kutunga na kusahihisha Mitihani
 Kufanya Utafiti utakosaidia kutoa majibu kwa matatizo/hangamoto mbalimbali katika jamii inayoizunguka chuo
 Kutoa Ushauri juu ya kuboresha Taaluma chuoni na kuendeleza Mafunzo nje ya chuo
32.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu mafunzo ya stashahada ya kilimo kutoka vyuo vya ufundi vinavyotambuliwa na Serikali.
32.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi.
33.0 MKUFUNZI MSAIDIZI DARAJA LA II – UCHORAJI NA UREMBAJI (PAINTING AND DECORATION) - (NAFASI 2)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Wakufunzi wasaidizi hawa watafanya kazi ya kufundisha masomo ya uchoraji na Urembaji katika vyuo vya maendeleo ya wananchi Tanzania Bara
33.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la uchoraji na urembaji katika vyuo vya maendeleo ya wananchi.
 Kutayarisha mpango wa kazi wa Mafunzo
 Kupima Maendeleo ya Wanachuo katika nadharia na vitendo
 Kutunza vifaa vya kufundishia
 Kufanya na kutoa taarifa za Utafiti
 Kutoa Ushauri wa kitaalam
 Kuandaaa kanuni na taratibu za kusimamia Mitihani chuoni
 Kutunga na kusahihisha Mitihani
 Kufanya Utafiti utakosaidia kutoa majibu kwa matatizo/changamoto mbalimbali katika jamii inayoizunguka chuo
 Kutoa Ushauri juu ya kuboresha Taaluma chuoni na kuendeleza Mafunzo nje ya chuo.
33.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu mafunzo ya stashahada ya ufundi katika fani ya uchoraji na Urembaji kutoka vyuo vya ufundi vinavyotambuliwa na Serikali.
33.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi.
34.0 MKUFUNZI MSAIDIZI DARAJA LA II – USEREMALA (CARPENTRY AND JOINERY) - (NAFASI 6)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Wakufunzi wasaidizi hawa watafanya kazi ya kufundisha somo la useremala katika vyuo vya maendeleo ya wananchi Tanzania Bara
34.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la useremala katika vyuo vya maendeleo ya wananchi.
 Kutayarisha mpango wa kazi wa Mafunzo
 Kupima Maendeleo ya Wanachuo katika nadharia na vitendo
 Kutunza vifaa vya kufundishia
 Kufanya na kutoa taarifa za Utafiti
 Kutoa Ushauri wa kitaalam
 Kuandaaa kanuni na taratibu za kusimamia Mitihani chuoni
 Kutunga na kusahihisha Mitihani
 Kufanya Utafiti utakosaidia kutoa majibu kwa matatizo/hangamoto mbalimbali katika jamii inayoizunguka chuo
 Kutoa Ushauri juu ya kuboresha Taaluma chuoni na kuendeleza Mafunzo nje ya chuo
34.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu mafunzo ya stashahada ya ufundi katika fani ya Useremala kutoka vyuo vya ufundi inavyotambuliwa na Serikali.
34.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi.
35.0 MKUFUNZI MSAIDIZI DARAJA LA II – UFUNDI CHUMA NA MABOMBA ( WELDING AND PLUMBING) - (NAFASI 12)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Wakufunzi wasaidizi hawa watafanya kazi ya kufundisha somo la ufundi chuma na bomba katika vyuo vya maendeleo ya wananchi Tanzania Bara
35.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha Masomo ya uungaji vyuma na ufundi bomba katika vyuo vya maendeleo ya wananchi.
 Kutayarisha mpango wa kazi wa Mafunzo
 Kupima Maendeleo ya Wanachuo katika nadharia na vitendo
 Kutunza vifaa vya kufundishia
 Kufanya na kutoa taarifa za Utafiti
 Kutoa Ushauri wa kitaalam
 Kuandaaa kanuni na taratibu za kusimamia Mitihani chuoni
 Kutunga na kusahihisha Mitihani
 Kufanya Utafiti utakosaidia kutoa majibu kwa matatizo/hangamoto mbalimbali katika jamii inayoizunguka chuo
 Kutoa Ushauri juu ya kuboresha Taaluma chuoni na kuendeleza Mafunzo nje ya chuo
35.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu mafunzo ya stashahada ya ufundi katika fani ya ufundi chuma na bomba kutoka vyuo vya ufundi inanvyotambuliwa na Serikali
35.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi.
36.0 MKUFUNZI MSAIDIZI DARAJA LA II – UFUNDI MAGARI (MOTOR VEHICLE MECHANICS) - (NAFASI 8)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Wakufunzi wasaidizi hawa watafanya kazi ya kufundisha somo la ufundi magari katika vyuo vya maendeleo ya wananchi Tanzania Bara
36.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundisha somo la umakenika katika vyuo vya maendeleo ya wananchi.
 Kutayarisha mpango wa kazi wa Mafunzo
 Kupima Maendeleo ya Wanachuo katika nadharia na vitendo
 Kutunza vifaa vya kufundishia
 Kufanya na kutoa taarifa za Utafiti
 Kutoa Ushauri wa kitaalam
 Kuandaaa kanuni na taratibu za kusimamia Mitihani chuoni
 Kutunga na kusahihisha Mitihani
 Kufanya Utafiti utakosaidia kutoa majibu kwa matatizo/hangamoto mbalimbali katika jamii inayoizunguka chuo
 Kutoa Ushauri juu ya kuboresha Taaluma chuoni na kuendeleza Mafunzo nje ya chuo
36.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu mafunzo ya stashahada ya ufundi katika fani ya ufundi magari kutoka vyuo vya ufundi inanvyotambuliwa na Serikali.
36.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi.
37.0 MKUFUNZI MSAIDIZI DARAJA LA II – UFUNDI VIATU(SHOE MAKING) - (NAFASI 2)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Wakufunzi wasaidizi hawa watafanya kazi ya kufundisha somo la ufundi viatu katika vyuo vya maendeleo ya wananchi Tanzania Bara
37.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundish somo la ushonaji viatu katika vyuo vya maendeleo ya wananchi.
 Kutayarisha mpango wa kazi wa Mafunzo
 Kupima Maendeleo ya Wanachuo katika nadharia na vitendo
 Kutunza vifaa vya kufundishia
 Kufanya na kutoa taarifa za Utafiti
 Kutoa Ushauri wa kitaalam
 Kuandaaa kanuni na taratibu za kusimamia Mitihani chuoni
 Kutunga na kusahihisha Mitihani
 Kufanya Utafiti utakosaidia kutoa majibu kwa matatizo/hangamoto mbalimbali katika jamii inayoizunguka chuo
 Kutoa Ushauri juu ya kuboresha Taaluma chuoni na kuendeleza Mafunzo nje ya chuo
37.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu mafunzo ya stashahada ya ufundi katika fani ya ufundi viatu kutoka vyuo vya ufundi inanvyotambuliwa na Serikali.
37.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi.
38.0 MSANIFU MAJENGO DARAJA LA II (ARCHITECT II ) - (NAFASI 2)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Wakufunzi wasaidizi hawa watafanya kazi ya kufundisha somo la Usanifu Majengo katika vyuo vya maendeleo ya Jamii
38.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundish somo la usanifu majengo katika vyuo vya maendeleo ya Jamii.
 Kutayarisha mpango wa kazi wa Mafunzo
 Kupima Maendeleo ya Wanachuo katika nadharia na vitendo
 Kutunza vifaa vya kufundishia
 Kufanya na kutoa taarifa za Utafiti
 Kutoa Ushauri wa kitaalam
 Kuandaaa kanuni na taratibu za kusimamia Mitihani chuoni
 Kutunga na kusahihisha Mitihani
 Kufanya Utafiti utakosaidia kutoa majibu kwa matatizo/hangamoto mbalimbali katika jamii inayoizunguka chuo
 Kutoa Ushauri juu ya kuboresha Taaluma chuoni na kuendeleza Mafunzo nje ya chuo
38.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu mafunzo ya Shahada ya Usanifu Majengo kutoka vyuo vinanvyotambuliwa na Serikali
38.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS E kwa mwezi.
39.0 MPIMA ARDHI DARAJA LA II (LAND SURVEYOR II ) - (NAFASI 2)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Wakufunzi wasaidizi hawa watafanya kazi ya kufundisha somo la Upimaji Ardhi katika vyuo vya maendeleo ya Jamii
39.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufundish somo la usanifu majengo katika vyuo vya maendeleo ya Jamii.
 Kutayarisha mpango wa kazi wa Mafunzo
 Kupima Maendeleo ya Wanachuo katika nadharia na vitendo
 Kutunza vifaa vya kufundishia
 Kufanya na kutoa taarifa za Utafiti
 Kutoa Ushauri wa kitaalam
 Kuandaaa kanuni na taratibu za kusimamia Mitihani chuoni
 Kutunga na kusahihisha Mitihani
 Kufanya Utafiti utakosaidia kutoa majibu kwa matatizo/hangamoto mbalimbali katika jamii inayoizunguka chuo
 Kutoa Ushauri juu ya kuboresha Taaluma chuoni na kuendeleza Mafunzo nje ya chuo
39.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu mafunzo ya Shahada ya Upimaji wa Ardhi kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali
39.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS E kwa mwezi.
40.0 FUNDI SANIFU DARAJA LA II-KOMPYUTA (TECHNICIAN II-COMPUTER ) NAFASI -2
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Mafundi Sanifu hawa watafanya kazi ya matengenezo madogomadogo ya kompyuta za wizara
40.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kuainisha matatizo mbalimbali ya Komputa na kushauri kuhusu matengenezo.
 Kutengeneza Komputa.
 Kuunganisha na kufunga Kompyuta mpya pindi zinapoletwa Wizarani
40.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu Stashahada ya Ufundi Kompyuta (Computer Engineering) kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali
40.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi.
41.0 KATIBU MUHTASI DARAJA LA III (PERSONAL SECRETARY III ) NAFASI 20
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Makatibu muhtasi hawa watafanya kazi ya kupiga chapa katika vyuo vya maendeleo ya wananchi
41.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kupokea wageni wanaofika katika ofisi ya Mkuu wa chuo
 Kupiga chapa nyaraka mbalimbali za Mkuu wa Chuo
 Kupiga chapa za mihtasari ya vikao vya chuo vikiwemo Bodi ya chuo, Menejimenti ya chuo, Baraza la wafanyakazi wa chuo nk.
 Kupiga chapa majaribio mbalimbali na matokeo ya wanachuo.
 Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Chuo
41.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu uhazili katika ngazi ya cheti (Secretarial) kutoka vyuo vya Utumishi wa Umma na vyuo vingine vinavyotambuliwa na Serikali
41.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi
42.0 MPISHI DARAJA LA II (COOK II ) NAFASI - 5
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Wapishi hawa watafanya kazi ya kuwapikia wanachuo katika vyuo vya maendeleo ya wananchi
42.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kuandaa chakula cha wanachuo kulingana na Menyu na idadi ya wanachuo
 Kupika chakula cha wanachuo
 Kutoa ushauri kwa uongozi wa chuo kuhusu chakula cha wanachuo.
 Kusimamia jiko.
42.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu mafunzo yacheti yasiyopungua mwaka mmoja katika fani ya food Production kutoka vyuo vinavyotambuliwa na serikali .
42.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi
43.0 MHUDUMU WA JIKONI (KITCHEN MESS ATTENDANT II) NAFASI-13
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Wahudumu hawa watapika chakula cha wanachuo chini ya usimamizi wa wapishi katika vyuo vya maendeleo ya wananchi
43.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kuandaa chakula cha wanachuo kulingana na Menyu na idadi ya wanachuo
 Kupika chakula cha wanachuo
 Kufanya usafi wa jiko.
 Na kazi nyingine atazopangiwa na mpishi/wasimamizi wao.
43.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye cheti cha mtihani wa kitado cha nne na kufuzu mafunzo si chini ya mwaka mmoja katika fani ya Food and Beverages kutoka kwenye vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.
43.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGOS A kwa mwezi
44.0 MHUDUMU WA OFISI II (OFFICE ASSISTANT II ) NAFASI -10
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Wahudumu hawa watafanyakazi za uhudumu katika ofisi ya Mkuu wa chuo katika vyuo vya maendeleo ya wananchi
44.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufungua na kufunga milango ya ofisi
 Kufanya usafi wa ofisi.
 Kupeleka vifurushi na barua
 Kuhudumia miradi ya mafunzo chuoni.
44.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofaulu vizuri katika masomo ya Kiingereza, Kiswahili na Hisabati.
44.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGOS A kwa mwezi
45.0 WALINZI (SECURITY GUARDS) NAFASI -20
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Walinzi hawa watafanyakazi ya kulinda chuo na mali zake mchana na usiku katika vyuo vya maendeleo ya wananchi
45.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kulinda chuo na mali zake.
 Kukagua mizigo inayoingia na kutoka ndani ya eneo la chuo.
 Kutoa taarifa za usalama wa chuo kwa uongozi wa chuo kwa kufuata miongozo, kanuni na taratibu zilizopo chuoni.
 Kutoa mapendekezo ya namna ya kuimarisha usalama wa chuo na mali zake kwa uongozi wa chuo.
45.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne/sita waliofuzu mafunzo ya mgambo.
45.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGOS A kwa mwezi
46.0 AFISA ELIMU MSAIDIZI DARAJA LA III (ASSISTANT EDUCATION OFFICER GRADE III) – (NAFASI 10)
Nafasi hzi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto.Walimu hawa watafundisha masomo katika moja wapo ya fani zifuatazo: Ujenzi (civil engineering),U

Show more